TIMU YA MADAKTARI KUTOKA CUBA NA ZANZIBAR KUTOA TAARIFA YA TAFITI ZAO HUKO KATIKA SKULI YA AFYA MBWENI

Timu ya Madaktari kutoka CUBA na Zanzibar waliowasilisha  tafiti mbali mbali za maradhi wakiwa na Viongozi wa Serikali ya Zanzibar (aliyekaa  katikati ) , Waziri wa Afya  Hamad  Rashid(  kushoto) Waziri wa Elimu Riziki Pembe Juma  na Balozi wa CUBA  Profesa Lucas Domingo  huko Skuli ya Afya Mbweni Zanzibar

Waziri wa Afya Hamad Rashid Mohamed imesema Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar itaendelea kuimarisha mashirikiano na nchi mbali mbali ili kuwapatia huduma za matibabu  wananchi wa Zanzibar

Hayo ameyasema leo huko katika Skuli ya Afya Mbweni wakati  wa Mkutano wa Madaktari wa Cuba na  Zanzibar  wakati  walipowasilisha Tafiti zao za maradhi mbali mbali  waliyoyafanyia uchunguzi ambayo yameonekana kushamiri duniani  kote na kupatiwa huduma za  matibabu.

Amesema Serikali ya Jamhuri ya Muungano waTanzania na Serikali ya Zanzibar ina mashirikiano makubwa na Serikali ya Cuba  na ya muda mrefu kwa lengo la kuboresha huduma za tiba kwa  maradhi  sugu ambayo  yanaikabili jamii.

Waziri wa Afya Hamad Rashid Mohamed (aliyesimama) akitoa shukrani kwa Madaktari wa Cuba pamoja na Madaktari wa Zanzibar kwa kufanya Utafiti wa Maradhi mbali mbali na kuweza kuguduwa tiba ambayo itawasaidia Wananchi wa Zanzibar kushoto Waziri wa Elimu Riziki Pembe Juma na Balozi wa CUBA Profesa Lucas Domingo katika warsha ya siku moja iliyofanyika huko Skuli ya Afya Mbweni Zanzibar

Aidha alisema  kuwa tafiti zinajionyesha ugunduzi wa tiba  utasaidia wagonjwa kurudia katika hali zao za kawaida pamoja na kuepukana na ulemavu usiotarajiwa hasa kwa wale wagonjwa wa sukari.

Alieleza kuongezaka kwa  wataaluma  nchini kutoka katika nchi tofauti kutasaidia mashirikiano ya kimatibabu na kuengeza ujuzi kwa Madaktari Wazalendo jambo ambalo  litasaidia  kuimarisha huduma za kimatibabu nchini.

Nae Mkuu wa Skuli ya Afya Suza Salum Seif  Salum akielezea utafiti kuhusu kudhibiti mazalia ya mbu alisema kuwa ongezeko kubwa  la mazalio ya mbu linatokana na uchafu wa mazingira katika maeneo  mbali mbali ya mji hasa  katika  baadhi ya mitaa ambayo  hutuwama maji na kusababisha  mazalio ya mbui maeneo ambayo yameonyesha kuwepo na mazalio mengi  ni  kikwajuni juu na bondeni

” Wizara ya Afya  kwenye kitengo  chetu cha kuondosha maradhi kinachukua juhudi za kuwaangamiza mbu hao ambao husababisha maradhi ya Malaria, homa ya manjano na pia homa ya kinyungu’nya na kuhakikisha wanapotea kabisa.”,alisema DK,Salum.

Msaidizi wa Skuli ya Afya , Amina Abdulkadir akitoa maelezo ya historia ya uunguzi na ukunga Zanzibar kwa Madaktari kutoka Jamhuri ya CUBA pamoja na Washiriki mbali mbali wakiwemo Viongozi wa Serikali ya CUBA na Zanzibar waliohudhuria katika Warsha ya utafiti huko katika ukumbi wa Chuo cha Afya Mbweni Zanzibar

 Kwa upande wa Msaidizi wa  Skuli ya Afya  Mbweni Amina Abdulkadir Ali wakati akiwasilisha mada ya uuguzi  na wakunga alisema   inapaswa  wauguzi  kuzingatia mambo matatu  muhimu katia kutoa matibabu kwa wagonjwa kwanza kichwa mikono na moyo ,kwa kuweza kuwa na moyo wa huruma na kutumia lugha nzuri  wakati wa kuhudumia  wagonjwa .

hata hivyo alisema kada ya uuguzi na ukunga imeweza kutimiza miaka 200 kwa sasa hivyo wataitumia kuisherehekea kwa kutoa elimu kwa wauguzi na wakunga wa  kila Wilaya ili waweze kufanya kazi zao kwa ufanisi zaidi.

Mada zilowasilishwa ambazo zimefanyiwa utafiti na Madaktari kutoka Cuba ni pamoja  na kensa ya kizazi, ziwa ,kisukari na maradhi mengine yaliyo sugu  kupatiwa uvumbuzi.

 Mkutano wa Timu ya Madaktari kutoka CUBA ni wa mara ya tatu kufanyika Zanzibar kwa lengo la  kubadilishana utaalamu wa kimatibabu.

Loading