WAZIRI WA AFYA HAMAD RASHID MOHAMED AFANYA ZIARA KATIKA HOSPITALI YA WILAYA KIVUNGE

Waziri wa Afya Hamad Rashid Mohamed akiwa katika Ziara ya  kutembelea Hospitali ya Kivunge Wilaya ya Kaskazini “A” Unguja (kushoto) Daktari dhamana wa Hospitali hiyo Tamim Hamad Said.

WAZIRI wa Afya Hamadi Rashid Mohammed amesema amefurahishwa na ujenzi unaoendelea huko katika Hospital ya Kivunge katika jengo la mama na mtoto .

Hayo ameyasema huko Hospital ya Kivunge wakati alipokuwa akifanya ziara ya jengo hilo ambalo linatarajiwa kumalizika ifikapo January mwakani.

Amesema malengo ya ziara  ni kuangaliya jinsi ujenzi unavyoendelea na hatua  iliyofikia   ikiwa ni miongoni mwa miradi ya maendeleo inayosimamiwa na Serikali ya Mapinduzi.

Aidha amesema Serikali  itahakikisha jengo litakapokwisha na kufunguliwa vifaa vyote vya huduma  ya mama na mtoto viweze kukamilika na kuanza huduma hizo mara moja.

“Jengo hili likimalizika liwe na vifaa vyote ili likifunguliwa huduma zianze mara moja”, alisema Waziri huyo.

Wakati huo huo Waziri Hamad alitembelea Hospitali ya Cotage ya kivunge na kujionea changamoto zinazoikabili ikiwemo upungufu wa baadhi ya vifaa vya uchunguzi  na upungufu wa madaktari.

Vile vile ameahidi katika ziara yake hiyo atazifanyiya ufumbuzi changamoto zinazoikabili Hospitali hiyo ili huduma ziendelee kutolewa kwa wananchi.

Aidha sehemu alizozitembelea ni pamoja na wadi ya wazazi, sehemu ya kuhifadhia dawa  na kuwasikiliza shida zao wananchi.

Nao wananchi wameishukuru Wizara ya Afya pamoja na Serikali ya Mapinduziya Zanzibar kwa kuwahudumia vyema wakati wot wanapohitaji huduma katika hospital hiyo.

Mkandarasi kutoka Kampuni ya WCEC LIMITED Edwin Shittindi akionyesha Jengo jipya la Hospitali ya Wilaya Kivunge ya Mama na Mtoto na kutoa maelezo kwa Waziri wa Afya Hamad Rashid Mohamed juu ya Ujenzi unaoendelea huko Wilaya ya Kaskazini “A”.

Nae  Mkandarasi Edwin Shittindi  wa Kampuni ya WCEC Limited inayoshughulikia jengo hilo amesema ujenzi  unaendelea vizuri  mbali na changamoto wanazokumbana nazo .

Amesema changamoto hizo ni pamoja na mchanga ambao ulikuwa ukipatikana kwa shida na kuishukuru Wizara ya Afya na kushirikiyana na Wizara ya Kilimo kwa kuwapatia kibali na kupatikana huduma hiyo kwa urahisi.

Jengo hilo linalotarajiwa kumalizika kwake January mwakani limegharimu zaidi ya  Bilioni 3 na Milioni mia tatu.

Loading